Utafiti uliofanywa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udsm)
umebaini kuwa mfumo wa uongzi wa nyumba kumi katika Serikali za mitaa ni
suluhisho la migogoro kwa kuwa unawapa nguvu vijana kushiriki mapambano dhidi
ya uhalifu
Utafiti huo uliofanyika katika Mikoa saba umebaini kuwa
kupitia mpango huo ambao ulikuwapo tangu miaka ya 1970 na kuasisiwa na Mwalimu
Julius Nyerere unaweza kuongeza uhusishwaji wa vijana katika masuala ya kijamii
Akizindua Utafiti huo leo Agosti 23 , Naibu Katibu Mkuu wa
Wizara ya Elimu,S ayansi na Teknolojia Dk.Ave Maria Semakafu amesema jamii
haipaswi kuwaona vijana kama chanzo cha migogoro na badala yake iwe ni mbadala
wa matatizo
"Vijana ni sehemu kubwa ya watu duniani na wamekuwa
waathirika wakubwa wa vita, ukatili, usalama na ulinzi lakini wanaweza kuwa
njia ya utatuzi wa mambo haya,"amesema
Amesema wizara ya elimu imeanzisha mfuko wa kuwawezesha
vijana kupitia sekta zisizo rasmi ili kuondoa wimbi la vijana wasio na ajira
ili kupunguza uhalifu
Mtafiti Mkuu wa utafiti huo, Profesa Benadetha Killian
amesema hali inaonyesha kuwa nyumba kumi imekuwa msaada mkubwa katika
usuluhishi kwenye ngazi za chini
Amesema katika maeneo ambayo yamekumbwa na migogoro mikubwa
kama Kibiti na Rufiji utafiti umebaini kuwa hakuna uongozi wa nyumba kumi ambao
ungeweza kuleta suluhu za viashiria vya migogoro
"Mgogoro wa Kibiti umedumu kwa takribani miaka miwili
lakini ukiangalia hakukuwa na Uongozi wa nyumba kumi ambao ni rahisi kufikiwa
pale watu wanapohitaji msaada hasa usuluhishi,"amesema
Utafiti huo unapendekeza Serikali ya nyumba kumi kutumika
kama taasisi rasmi ya usuluhishi kwa sababu ni rahisi kuwafikia viongozi wake
kutokana na udogo wa eneo
"Mfumo wa nyumba kumi bado una nguvu na haujafa.Kupitia
nyumba kumi unakuta vijana wanashiriki katika ulinzi shirikishi ambao unasaidia
kupunguza uhalifu,"amesema Mtafiti huyo
Utafiti huo umefanyika katika kipindi cha Julai hadi
Septemba mwaka jana ukihusisha Mikoa ya Tanga,Kagera,Pwani,Mtwara,Arusha,Mwanza
na Zanzibar
Utafiti: Uongozi wa nyumba kumi kumi suluhisho bora la migogoro
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 23, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment