Katibu Mkuu UWT akemea wanaokejeli uteuzi wa wanawake


Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake wa chama cha Mapinduzi (UWT) Queen Mlozi ameitaka jamii kukemea kauli za kejeli zinazotolewa pindi mwanamke anapoteuliwa katika nafasi ya uongozi

Mlozi ameyasema hayo leo Agosti 23 jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio yaliyofikiwa katika utekekezaji wa ilani ya CCM

Amesema anasikitishwa na kauli hizo kwa kuwa zinalenga kuwakatisha tamaa wanawake na kuwafanya washindwe kujiamini.

Mlozi amesema kwa mwenendo huo upo uwezekano hata anayefanya uteuzi akakata tamaa kwa kuwa akiteuliwa mwanamke kauli zisizofaa zinatolewa

"Wanawake tuwe mstari wa mbele kukemea  kauli hizi kwa kuwa si nzuri na zinalenga kuturudisha nyuma

"Kwanza tujiulize kwanini kejeli zinaibuka akiteuliwa mwanamke, tuelimishane, tuzungumze na tukemee haya kwa umoja wetu,” amesema

“Ni lazima ifike mahali tuseme hapana itafika wakati hata anayetuteua atapata ukakasi. Tusikatishane tamaa katika vitu vya msingi."ameongeza

Mlozi ametumia fursa hiyo kumuomba Rais John Magufuli kuendelea kuwaamini na  kuwateua wanawake kwa kuwa wanaweza kufanya kazi kwa uaminifu mkubwa

Katibu Mkuu UWT akemea wanaokejeli uteuzi wa wanawake Katibu Mkuu UWT akemea wanaokejeli uteuzi wa wanawake Reviewed by KUSAGANEWS on August 23, 2018 Rating: 5

No comments: