Chadema kutumia wabunge wake kulinda kura uchaguzi mdogo Septemba 16


Chadema kanda ya kati kimesema kitawaumia wabunge wake kulinda kura wakati wa uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya Kizota jijini hapa unaotarajiwa kufanyika Septemba 16, 2018

Hayo yamesemwa leo Agosti 23 na Katibu wa Chadema kanda ya kati, Iddi Kizota muda mfupi baada ya mgombea wa chama hicho kurudisha fomu ya kugombea udiwani

Amesema wamefikia uamuzi huo baada ya baadhi ya mawakala wanaowekwa vituoni kujiondoa siku ya kupigra kura

"Ikiwezekana tutatumia hata wabunge na ukiangalia uchanguzi unafanyika Septemba 16,2018 kipindi ambacho Bunge linaendelea na vikao vyake  basi wabunge 19 tutaweza kuwapata,"

"Katika kata yetu ya Kizota tuna vituo vya kupigia kura 19 hivyo hao wabunge 19 ni kwa ajili ya kuwa mawakala kwenye vituo vya kupigia kura," amesema Kizota

Kwa upande wake mgombea udiwani wa kata ya Kizota  kupitia Chadema Omary Bangababo amesema kuwa ameamua kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo ili kuwatumikia wananchi ikiwa ni pamoja na kutatua kero ya wanafunzi wa shule ya sekondari Kizota ya kutokuwa na maabara

Kwa upande wake, Mtendaji wa Kata ya Kizota Loyce Mrefu amesema hada sasa wawakilishi  wote vyama sita waliochukua fomu kwa nafasi hiyo ya udiwani wamekwisharejesha fomu zao

Waliorudisha fomu ni Jamali Ngalya (CCM),  Salum Salum (CUF), Omary Bangababo (Chadema), Jacklin Msajila (UPDP), Aziz Abas (NCCR- Mageuzi) pamoja na Peter Malya (NLD).

Chadema kutumia wabunge wake kulinda kura uchaguzi mdogo Septemba 16 Chadema kutumia wabunge wake kulinda kura uchaguzi mdogo Septemba 16 Reviewed by KUSAGANEWS on August 23, 2018 Rating: 5

No comments: