Apandishwa kizimbani kwa kumpa mimba mwanafunzi


Mkazi wa Vingunguti, Seleman Mohamed (18), amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, kujibu shtaka la kumpa mwanafunzi mimba

Mohamed amepandishwa mahakamani hapo leo Agosti 23, mbele ya Hakimu Mkazi Eliarusia Nassary na kusomewa shtaka moja la kumpa mimba mwanafunzi mwenye umri wa miaka 17.

Wakili wa Serikali, Ashura Mzava, amedai mshitakiwa alitenda kosa hilo kati ya Aprili na Juni, 2018 eneo la Vingunguti wilayani Ilala

Mshtakiwa anadaiwa siku hiyo ya tukio huku akijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria, alimpa mimba mwanafunzi mwenye umri wa miaka 17.

Hata hivyo, mshtakiwa baada ya kusomewa shtaka linalomkabili, alikana shitaka hilo ambapo upande wa mashitaka ulidai upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika na hivyo kuomba tarehe nyingine ya kutajwa

Hakimu Eliarusia ametaja masharti ya dhamana ambayo ni wadhamini wawili mmoja kati yao awe mwajiriwa watakaosaini dhamana ya Sh1milioni kila mmoja

Mshtakiwa alishindwa kutimiza masharti ya dhamana na kurudishwa rumande hadi Septemba 4, mwaka huu, kesi  yake itakapotajwa

Katika hatua nyingine, Athuman Mohamed (18), amefikishwa mahakamani hapo akikabiliwa na shtaka la kukutwa na dawa za kulevya aina ya bangi zenye uzito wa kilogramu 3.55
Akisomewa hati ya mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Flora Mujaya, wakili wa Serikali Sylvia Mitanto, alidai mshtakiwa alikutwa na kiasi hicho cha bangi Agosti 7, 2018, eneo la Kivule Matembele wilayani Ilala

Mshitakiwa alikana shitaka hilo na upande wa mashtaka walidai kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika na hivyo kuomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa

Hakimu Flora ametaja masharti ya dhamana kuwa, mshtakiwa anatakiwa kuwa na wadhamini wawili ambapo mmoja kati yao awe na barua kutoka sekta yoyote inayotambulika watakaosaini  dhamana Sh 1milioni moja kila mdhamini

Apandishwa kizimbani kwa kumpa mimba mwanafunzi Apandishwa kizimbani kwa kumpa mimba mwanafunzi Reviewed by KUSAGANEWS on August 23, 2018 Rating: 5

No comments: