Chama cha Wanasheria nchini (TLS) kimepinga Marekebisho ya
Sheria ya TLS yanayolenga kuwakataza watumishi wa Serikali na viongozi wa
kisiasa kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika chama hicho kikieleza kuwa
marekebisho hayo yanawabagua wanachama.
Akizungumza leo
Agosti 24 wakati wadau wa masuala ya sheria wakitoa maoni yao kwa Kamati ya
Bunge ya Katiba na Sheria, mwakilishi wa TLS, Jebra Kambole alisema marekebisho
hayo pia yanalenga katika kumfanya mwanachama mmoja kuwa na nguvu kuliko
wengine
TLS ilikuwa ikitoa maoni kuhusu Muswada wa Sheria namba
mbili wa mwaka 2018
“Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni mwanachama wetu,
anapelekewa kanuni kwa ajili ya kupitisha ni wazi hapa mwanachama huyu anakuwa
na nguvu kuliko wanachama wengine,”alisema
Alitaja sababu nyingine ya kupinga mapendekezo hayo ni pale
Mwanasheria Mkuu wa Serikali AG atakapopewa mamlaka ya kupitisha kanuni, chama
hicho hakitakuwa na uhuru wa kujiendesha
Mbunge wa Malindi (CUF) Ally Saleh alitaka TLS kiwashawishi
kwa nini mkono wa Serikali usiingie katika chama hicho
Hoja ya Saleh iliungwa mkono na mwenyekiti wa kikao hicho,
Dk Damas Ndumbaro ambaye alikitaka chama hicho wakati kinajibu swali hilo kutoa
mifano ya bodi nyingine ambazo Serikali haitengenezi kanuni
“Pia mmesema kuna ubaguzi sasa ikitokea siku Rais anagombea
uraisi je mtamruhusu? Tuchukue mfano Rais Magufuli ni mwanachama wa TLS na
uchaguzi uko Februari mwakani mtamruhusu agombee? Kama sheria inaruhusu nani
atamzuia?” Alihoji Dk Ndumbaro ambaye pia ni mbunge wa
Dk Ndumbaro ambaye pia ni mwanachama wa siku nyingi wa TLS
alisema kumekuwa na mabadiliko ya majukumu ya TLS kutoka katika kushughulikia
taaluma na kujiingiza katika siasa
Akijibu hoja hizo, Kambole alisema hawezi kuwa na jibu la
moja kwa moja kuhusu upitishaji wa kanuni za uendeshaji kwa bodi nyingine
lakini kuna tofauti kubwa kati yao na bodi nyingine za kitaaluma
“Huwezi kukuta daktari anakutana na daktari wa serikali
lakini sisi katika mashauri huwa tunakutana na AG sisi upande huu mwingine.
Lakini pia chama chetu hakina fungu lolote linalotoka Serikalini, ni michango
ya wanachama wenyewe,”alisema
Alisema iwapo mwanachama anayelipa michango yake ataomba
uongozi hata kama ni mtumishi wa Serikali atapigiwa kura sawa na wanachama
wengine
Akizungumzia hoja hiyo, Waziri wa Katiba na Sheria
Palamagamba Kabudi alisema sehemu ya 14 ya sheria hiyo inapendekeza kurekebisha
Sheria ya TLS, Sura ya 307
Alisema marekebisho hayo yanalenga kuweka vigezo ambavyo
vitatumika kwa wajumbe wa baraza na taratibu za kuzifuata wakati wa utungaji wa
kanuni zinazosimamia chama hicho
“Kwa ufupi mapendekezo ya marekebisho ya sheria hii yana
lengo la kuweka masharti ya kumtaka Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuzipitisha
kanuni zinazotungwa na chama kabla ya kuchapishwa. Pia kanuni hizo
zitachapishwa kwenye Gazeti la Serikali,”alisema
TLS chapinga marekebisho ya sheria yake
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 24, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment