Mwanafunzi afariki dunia, adaiwa kupigwa na radi


Mwanafunzi wa darasa la pili Shule ya Msingi Kagoma, Belina Bonifasi (9) mkazi wa kijiji cha Kagoma wilayani hapa mkoani Kagera amefariki dunia leo Ijumaa Agosti 24, 2018, ikielezwa kuwa amepigwa na radi

Akizungumza leo mzazi wa mwanafunzi huyo,  Renatus Pastory amesema mwanae alikutwa na umauti wakati akijiandaa kwenda shule baada ya radi kupiga dirishani

“Ameungua upande wa kulia wa mwili wake. Alikuwa akiandaliwa chai na mama yake ili aweze kwenda shule,” amesema

Mwalimu mkuu wa shule hiyo, Jeremiah Januari amesema mwanafunzi huyo  alikuwa miongoni mwa wanafunzi 115 wa darasa la pili shuleni hapo na kubainisha kuwa wamepokea taarifa za kifo hicho kwa mshtuko
Chanzo:Mwananchi
Mwanafunzi afariki dunia, adaiwa kupigwa na radi Mwanafunzi afariki dunia, adaiwa kupigwa na radi Reviewed by KUSAGANEWS on August 24, 2018 Rating: 5

No comments: