Serikali yawaondolea Wananchi Maafa yaliyokuwepo tangu Mkoloni


Wananchi wa kata ngaranaro jijini arusha wameanza kuondokana na Changamoto ya mafuriko iliyokuwa inawakabili kwa muda mrefu na Kuwasababishia wananchi hao hasara ya mali pamoja na Nyumba zao kubebwa na mafuriko kila  Mvua inaponyesha.

Akizungumza Mkuu wa wilaya ya Arusha Mjini Fabian Daqaro alipotembelea katika kata hiyo amekagua jinsi mtaro unavyojengwa amesema mpaka kukamilika kwake utagharimu Sh Milioni 295 .

Daqaro Amesema kuwa kipindi cha Mvua kulikuwa na changamoto kubwa za wananchi kuingiliwa na maji katika makazi yao hivyo kupitia ujenzi huo utarahisisha kutatua tatizo hilo  lililokuwepo kama hali ya hewa itaendelea kuwa nzuri na mvua za kawaida.

Pamoja na hayo amewataka viongozi  wa ngazi ya kata kuhakikisha wanasimamia kwa umakini ujenzi huo pamoja na kusimamia wananchi wasitupe taka katika mtaro huo unaojengwa kwa fedha nyingi.

Naye meneja wa mamlaka ya usimamizi wa barabara Mkoa wa Arusha Eng John Kalupale amesema kuwa urefu wa mtaro huo ni Mita 313 na utajengwa kwa miezi 2 lakini kutokana na kasi ya Mkandarasi pamoja na mafundi wanaofanya kazi hiyo itafanyika kwa mwezi mmoja na nusu.

Eng Kalupale amesema kuwa kila mwananchi anatakiwa kuwa kipao mbele kulinda miundombinu inayoletwa na serikali ambayo inamanufaa kwa wananchi wote kwa ujumla na kuunga mkono juhudi zilizopo kwa kuwa kuna baadhi wanaona kuwa ni kama kero kwa kuwa inapita maeneo yao.

Wananchi wa kata ya Ngarenaro wameishukuru serikali kwa kuwajengea mtaro huo kwasababu kila kipindi cha mvua kinapofika wengi huteseka kutokana na mafuriko kuingia katika makazi yao na wengine kuhama kipindi cha Mvua.

Serikali yawaondolea Wananchi Maafa yaliyokuwepo tangu Mkoloni Serikali yawaondolea Wananchi Maafa yaliyokuwepo tangu Mkoloni Reviewed by KUSAGANEWS on August 23, 2018 Rating: 5

No comments: