Rais Magufuli awashukuru watanzania


Rais John Magufuli amewashukuru watanzania na viongozi wa serikali waliojitokeza kumfariji wakati wa msiba wa dada yake, Monica Joseph Magufuli

Monica alifariki dunia Agosti 19 mwaka huu na kuzikwa Agosti 21 katika kijiji cha Mlimani, Chato, Geita

Rais Magufuli amesema upendo na ushirikiano uliooneshwa na kila aliyeguswa na kifo cha dada yake umemfariji kwa kiasi kikubwa yeye na familia nzima na umewatia nguvu na ustahimilivu katika kipindi kigumu cha majonzi

“Kifo cha Dada yangu Monica, kimesababisha huzuni na majonzi makubwa kwetu sisi wanafamilia kwa kuwa tulimtegemea kwa mengi na ndiye alikuwa akimlea Mama yetu  Suzana Ngolo Magufuli, lakini salamu za pole, maombi yenu na tulipowaona wengi mmekuja kuungana nasi kumsindikiza katika safari ya mwisho, tumefarijika sana na tumepata nguvu

“Kwa niaba ya familia naomba kuwashukuru sana nyote kwa moyo wenu wa upendo na maombi yenu, naamini mtaendelea kuungana nasi kumuombea dada yetu Monica apumzike mahali pema peponi, Amina” amesema Rais Magufuli

Rais Magufuli awashukuru watanzania Rais Magufuli awashukuru watanzania Reviewed by KUSAGANEWS on August 23, 2018 Rating: 5

No comments: