Mgombea wa Udiwani wa CCM Kata ya Mswakini wilayani Monduli,
Nanga Lenasira Mollel amepita bila kupingwa
Ofisa Uchaguzi Halmashauri ya wilaya ya Monduli, Meleji
Kuresoi amesema hadi leo saa 10 jioni hakuna mgombea wa upinzani aliyejitokeza
"Tulitangaza muda wa kuchukua fomu na kurejesha lakini
hadi leo jioni amechukua Lenasira pekee na kurejesha" amesema
Amesema kutokana na taratibu za uchaguzi zilivyo mgombea
huyo amepita bila kipingwa
Awali Diwani huyo alikuwa ni wa Chadema na alijiuzulu na
kujiunga na CCM na kuchukua fomu kutetea nafasi yake
Hadi sasa jumla ya madiwani 10 wa Chadema wilaya ya Monduli
wamejiuzulu na kujiunga na CCM
Kwa mujibu wa msimamizi wa uchaguzi Monduli, Stevin Ulaya
sasa halmashauri ya Monduli ambayo awali ilikuwa ya Chadema kutokana na kuwa na
madiwani 18 na CCM 9 tu imekuwa ya CCM
Kwa sasa CCM imekuwa na madiwani 17 huku Chadema ikibaki na
tisa
Mgombea udiwani wa CCM Monduli apita bila kupingwa
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 23, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment