Museveni: Sina uwezo kumtoa Bobi Wine


Rais Yoweri Museveni amesema kwamba, yeye kama mkuu wa nchi, hana mamlaka ya kumwachia huru Mbunge wa Kyadondo Mashariki, Robert Kyagulanyi pamoja na wenzake waliokamatwa na polisi

"Rais wa Uganda hana mamlaka kama hayo," amesema katika taarifa yake iliyofuatia mkasa uliotokea wakati wa uchaguzi mdogo wa Jimbo la manispaa ya Arua

"Mara mtu akikamatwa, akashtakiwa na kuwekwa mahabusu, ni mamlaka mbili tu ambazo zinaweza kuwatoa watu hao kwa namna yoyote," anasema Rais Yoweri Museveni

Katika taarifa ndefu aliyoitoa Jumatano, Museveni pia alilaani namna waandishi wa habari walivyopigwa na vyombo vya usalama

Katika taarifa iliyokuwa ujumbe kwa wananchi wa Uganda Museveni alisema, “Nimesoma maoni yenu kuhusiana na kauli yangu ya awali. Ninawashukuru nyote kwa kutoa maoni yenu. Hii ndiyo njia nzuri na yenye manufaa kwa kuwasiliana; hakuna haja ya vurugu na "fujo".

Hata hivyo, kuna kitu kimoja ambacho watu hawataki kukielezea katika maoni yao. Hicho ni suala la ukosefu wa ajira kwa vijana mijini na vijijini.

Hicho ni moja ya vipengele, ukweli ni kipengele kikuu, wanasiasa wasio na misingi (wanaojijali masilahi yao na wanaoweka kando taratibu zinazokubalika kufikia mafanikio) wanakitumia kuwashawishi vijana wetu kuingia kwenye na fujo,” alisema

Museveni: Sina uwezo kumtoa Bobi Wine Museveni: Sina uwezo kumtoa Bobi Wine Reviewed by KUSAGANEWS on August 24, 2018 Rating: 5

No comments: