Mahakama yampa ushindi Mnangagwa


Mahakama Kuu nchini Zimbabwe, imetupilia mbali kesi iliyofunguliwa na chama cha upinzani nchini humo, MDC ya kupinga matokeo ya uchaguzi yaliyompa ushindi, Emmerson Mnangagwa

“Katika uchunguzi wake Mahakama imebaini kuwa mlalamikaji ameshindwa kuonyesha ushahidi kamili na wa moja kwa moja kwamba uchaguzi uligubikwa na kasoro” amesema Jaji Mkuu Luke Malaba wakati akitangaza uamuzi huo katika mahakama ya Katiba, jijini Harare

Oktoba mwaka jana, Mnangangwa alimrithi Robert Mugabe aliyetawala Zimbabwe kwa zaidi ya miaka 37

Katika uchaguzi huo uliofanyika Agosti mwaka huu, Zanu-PF kilishinda kwa asilimia 50.8 ya kura zote na chama cha upinzani cha MDC kilipata asilimia 44.3 ya kura hizo

Katika kesi hiyo, majaji tisa wakiongozwa na Jaji Mkuu Malaba, walitoa uamuzi huo huku ulinzi katika eneo la Mahakama ukiimarishwa

Kwa mara ya kwanza nchini humo, kesi hiyo ilirushwa moja kwa moja na televisheni ya taifa

Mahakama yampa ushindi Mnangagwa Mahakama yampa ushindi Mnangagwa Reviewed by KUSAGANEWS on August 24, 2018 Rating: 5

No comments: