Wanasiasa watakiwa kuacha kutetea wanaoharibu mazingira


Wanasiasa wametakiwa kuacha kutetea wananchi wanaovamia maeneo yaliiyotengwa ikiwamo vyanzo vya maji kwa kuwa wanaharibu mazingira

Hayo yameelezwa leo na Makamu wa Rais, Samia Suluhu, kwenye kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mazingira na maonyesho ya ubunifu, leo Juni 5, yaliyofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini hapa

“Tunapaswa kukuza uelewa na utashi  wa kisiasa kwa uhifadhi wa mazingira kuna maeneo wananchi wanavamia kwa makusudi, wanatokea wabunge na madiwani wanawatetea,"amesema
Mama Samia amesema kila mmoja anapaswa kutafakari namna bora ya kukabiliana na changamoto katika utunza mazingira ili maisha yaendelee

"Mapambano ya uharibifu wa mazingira siyo jukumu la Serikali pekee, bali kila mmoja ashiriki,"amesema

Waziri wa Mazingira ofisi ya Makamu wa Rais, January Makamba akizungumza kabla ya kumkaribisha Mama Samia,amesema amedhamiria kuwatumia vyema viongozi wa dini  katika kuhamasisha utunzaji wa mazingira. 

“Wenzetu hawa wana watu,  hivyo watatusaidia kuhubiliri uhifadhi wa mazingira,"amesema  Waziri Makamba 

Amesema kuna matumizi mkubwa ya nishati ya mkaa ambapo wakazi  wa Mkoa wa Dar es salaam wanatumia kwa asilimia 70 wakati  tafiti zikionyesha mkoa huo upo hatarini kuwa jangwa.
Wanasiasa watakiwa kuacha kutetea wanaoharibu mazingira Wanasiasa watakiwa kuacha kutetea wanaoharibu mazingira Reviewed by KUSAGANEWS on June 05, 2018 Rating: 5

No comments: