Watuhumiwa saba wa uhamiaji haramu wakamatwa Chalinze


Wahamiaji saba raia wa Ethiopia wamekamatwa Kijiji cha Pingo Chalinze mkoani Pwani baada ya kukutwa wakiwa wamejificha kwenye jengo la nyumba ambayo bado haijaisha ujenzi wake (pagale) 

Akizunguma leo Juni 5, Kamanda wa Polisi, Pwani Jonathan Shanna amesema raia hao pia wanashikiliwa kwa kosa la kuingia nchini bila kibali na walikamatwa alasiri Juni 04 kijiji hapo

Shanna amesema wahamiaji hao walioonekana kuwa na njaa wamedai walikuwa wanasafiri kuelekea Msumbiji kutafuta maisha kwa madai kuwa nchini kwako hali si shwari na kuna mapigano.
Watuhumiwa saba wa uhamiaji haramu wakamatwa Chalinze Watuhumiwa saba wa uhamiaji haramu wakamatwa Chalinze Reviewed by KUSAGANEWS on June 05, 2018 Rating: 5

No comments: