Wakuu wa manunuzi, uhasibu wasimamishwa Kenya

Nairobi, Kenya. Rais Uhuru Kenyatta Jumatatu aliwasimamisha wakuu wote wa Idara za Manunuzi ya Umma na Vitengo vya Uhasibu katika wizara zote wakisubiri kufanyiwa upya uhakiki, hatua inayolenga kung’oa ufisadi kwa watumishi wa umma serikalini

Hatua hii imekuja siku chache tangu Rais Kenyatta atoe tangazo wiki iliyopita kwamba wote wanaoshikilia ofisi za umma wajiandae kufanyiwa uhakiki ili kujua uaminifu wao. Kenyatta aliwaonya wakuu hao kwamba wale wote watakaoshindwa kufikia vigezo vilivyowekwa vya uhakiki watasimamishwa na baadaye kushtakiwa ikiwa watapatikana wana makosa ya ukiukwaji wa sheria za manunuzi ya umma

Pia, hatua hii imekuja katika kipindi ambacho watu kadhaa wamekamatwa wakituhumiwa kuhusika na kashfa zilizoandikwa sana kwenye vyombo vya habari na kuwaudhi wananchi hali iliyomlazimu rais kuchukua hatua hiyo

Watu 54 washtakiwa

Watu 54, wakiwemo katibu mkuu wa utumishi wa umma, walikamatwa na kushtakiwa wiki iliyopita wakidaiwa kuhusika katika wizi kutoka Shirika la Taifa la Huduma kwa Vijama (NYS

Shirika hilo lililoko chini ya Wizara ya Vijana ambalo lilianzishwa kwa lengo la kukabiliana na ukosefu wa ajira, linahusika katika kufundisha vijana kufanya kazi katika miradi tofauti kuanzia ujenzi hadi kudhibiti watu barabarani

Lakini kwa bahati mbaya, hazina ya NYS iliingiliwa na wahuni. Mwaka 2015, aliyekuwa Waziri wa Ugatuzi Anne Waiguru alijiuzulu baada shinikizo kutoka kwa wananchi kutokana na wizara yake kudaiwa kukubuhu katika rushwa, na yeye binafsi alihusishwa na wizi wa Sh791 milioni (dola 8 milioni) kutoka NYS. Lakini mwaka 2017 Waiguru alichaguliwa kuwa gavana wa Kaunti ya Kirinyaga katika mkoa wa kati
Wakuu wa manunuzi, uhasibu wasimamishwa Kenya Wakuu wa manunuzi, uhasibu wasimamishwa Kenya Reviewed by KUSAGANEWS on June 05, 2018 Rating: 5

No comments: