Nigeria. Jeshi Jumatatu lilisema kuwa
liliwaokoa wanawake 58 waliokuwa wakitumika kama watumwa wa ngono na Boko Haram
huko Modu Kimeri, eneo la Serikali ya mitaa katika Jimbo la Borno
Naibu Mkurugenzi wa Uhusiano na Uendeshaji
wa Kamandi ya Operesheni Lafiya Dole, Onyema Nwachukwu alisema mjini hapa
kwamba mbali ya wanawake hao, pia jeshi liliwaokoa watoto 75 na wanaume 15
Nwachukwu alisema wanawake hao waliokolewa
na askari wa Brigedi ya 21 wakishirikiana na Kikosi Kazi Maalumu cha Raia
kilichoandaliwa katika operesheni hiyo iliyopewa jina la Operesheni Lafiya Dole
"Jeshi liliwaokoa mateka hao katika
Operesheni Safishasafisha Jumapili ya Juni 3, 2018, ili kulisafisha kwa ujumla
eneo lote la Bama, Modu Kimeri na Gulumba Gana walikokuwa wakikaa magaidi wa
Boko Haram waliokuwa wakikimbia kutoroka vita vikali katika Visiwa vya Ziwa
Chad na mipaka ya kaskazini ya Jimbo la Borno
"Mateka waliokolewa, wamo wanaume 15,
wanawake 58 na watoto 75 waliogundulika wakati wakichujwa na kuhojiwa na askari
wa Operesheni Lafiya Dole na mashirika mengine ya usalama, kwamba magaidi ya
Boko Haram waliwadhalilisha kingono wanawake na waliwatumia kama watumwa wa
ngono," alisema
eshi laokoa wanawake watumwa wa ngono
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 05, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 05, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment