Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul
Makonda amesema ataanzisha operesheni ya usafi wa mazingira itakayoshirikisha
askari wa Jeshi la Kujenga Taifa 400 ili kuhakikisha jiji hilo linakuwa
safi tofauti na lilivyo sasa
“Naomba unifikishie salamu hizi kwa
Rais John Magufuli tutawakamata, hapa ni askari wa JKT (Jeshi la Kujenga Taifa)
400. Ziba masikio nataka niendeshe operesheni ili jiji linyooke na liwe
safi," amesema Makonda
Makonda ametoa kauli hiyo leo
Jumanne Juni 5 2018 wakati wa maadhimisho ya siku mazingira duniani ambayo
kitaifa yamefanyika viwanja vya Mnazi Mmoja na kuhudhuriwa na Makamu wa Rais
Samia Suluhu Hassan
Makonda amemweleza Samia kuwa
bado usafi katika jiji la Dar es Salaam ni tatizo na kwamba watu ni
wachafu na wanatia aibu
Makonda atatumia askari 400 wa JKT operesheni usafi wa mazingira Dar
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 05, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 05, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment