|
Dodoma. Mbunge wa Mbeya Mjini
(Chadema) Joseph Mbilinyi maarufu kama Sugu amemweleza Spika wa Bunge Job
Ndugai kuwa hawana Ilani za uchaguzi za CCM tu bali hata orodha ya ahadi
ambazo zimetolewa na chama hicho wakati wa uchaguzi mwaka 2020.
Akichangia bajeti ya Wizara ya
Fedha na Mipango kwa mwaka wa fedha 2018/19, Sugu amesema wakati yeye akiwa
gerezani Ndugai alitaka wabunge wote kupewa ilani ya uchaguzi ya CCM
“Sijui kama walipewa (Ilani)
lakini mimi nikuhakikishie mheshimiwa Spika kuwa hatuna ilani ya ccm tu bali
hata ahadi ambazo mmetoa wakati wa uchaguzi,”amesema
Akazitaja ahadi hizo ambazo ni
pamoja na laptop, Sh milioni 50 katika kila kijiji na elimu bure ambayo ipo
lakini ni janga tu
“Kuna watu walikuwa wanasema kuwa
elimu bure mmeiga kutoka kwa Chadema jambo ambalo ni zuri, lakini kwa jinsi
mnavyotekeleza ni kama kweli mmeichukua tu kutoka Chadema,”amesema
Pia amesema akiwa mjumbe wa Kamati
ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii wametembelea Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, na
kubaini kuwa hosteli zimejengwa kwa zaidi ya Sh54 bilioni si Sh10 bilioni
kama ilivyotamkwa
“Sijaona ripoti ya CAG (Mthibiti
na Mkaguzi Mkuu wa Serikali) kuhusu hili, watu wanang’ang’ana zimejengwa kwa
Sh 10 bilioni. Tunamdanganya nani? Kama fedha ni zetu kama
Taifa,”amesema
Amesema namba hazidanganyi kuna
tofauti kubwa kati ya Sh 10bilioni na Sh 54bilioni. Pia Sugu amemtaka Waziri
wa Fedha atakapojibu hoja za wabunge kueleza ni wapi zimeenda Sh1.5 trilioni
zilizohojiwa na CAG
“Hakuna mtu anayesema fedha kuwa
zimeibiwa, tunahoji zimekwenda wapi? Taifa hili si sebule ya familia si
tunapelekana tu,”amesema
|
|
Sugu: Tunazo ilani, ahadi za CCM
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 05, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 05, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment