Shekh mkuu wa mkoa wa Arusha Shaban Bin Juma amepongeza kikundi
cha friends of batuli ambacho kimejitolea misaada mbalimbali ya vyakula kwa
ajili ya wanawake wajane 21 wanaosali katika msikiti wa migungani ,pamoja na
vitabu vya madrasa kwa ajili ya watoto 78 wanaosoma katika msikiti huo kata ya
Sokoni One jijini Arusha.
Akizungumza Shekh Juma Amesema kuwa kundi hilo
lilichofanya ni ibada ambayo ndiyo inayompa mtu kuonekana ana roho ya namna
gani mbele ya watu kwa kuwa hata vitabu vitakatifu vimefafanua juu ya mtu
anayetoa msaada kwa asiyejiweza anapata dhawabu nyingi.
Amesema kuwa kundi hilo limetoa kitu ambacho kiko ndani
ya uwezo wao na wanaweza kuona kuwa ni jambo la kawaida lakini wametengeneza
mapenzi mema na jamii inayowazuunguka
“Jambo hili linajenga mapenzi mema katika jamii yetu na
maana yake tutakuwa tumeipa ulinzi miji yetu mitaa yetu na nchi yetu, haya
kadri yanavyofanyika ni mambo yanayokinga shari sidhani kama yupo mtu binadamu
aliye na akili aliyetendewa wema hata kidogo Yule aliyemtendea wema akawa adui
yake kupeana hidaya ni jambo linalotekekeza mapenzi katika jamii”Alisema Shekh
Juma
Ameongeza kuwa licha ya kuwa kikundi hicho ni watu wa
dini mbalimbali lakini hawakutanguliza udini wala ukabila bali wameungana na
kufanya utu ambao amesema hakuna Dini bila ubinadamu kwanza.
Kwa upande wa msemaji wa Friends of Batuli Bi Batuli
Kisaya amesema kuwa imekuwa ni desturi yao kusaidia watu wasiojiweza wakiwemo
watoto wanaoishi mazingira magumu pamoja na wajane ambapo ndiyo lengo kuu la
kundi hilo.
Batuli amesema licha ya kuwa na changamoto lakini
walichonacho kadri ya uwezo wao wanajitolea ambapo vitu hivyo walivyoto vina
dhamani ya shilingi laki saba na nusu
Nao akina mama wajane waliopata misaada hiyo wamelipongeza
kundi hilo ambapo wamesema kuwa maombi yao kwa mwenyezi Mungu ni kula vitu
halali ambavyo vinatoka kwenye mikono salama hivyo wanaamini Mungu amesikia
maombi yao
Shekh Mkuu awapongeza kundi la Friends Of Batuli kwa msaada waliotoa kwa Wajane.
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 03, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment