Wapagazi Wajitolea kukusanya chupa za plastiki jiji la Arusha


Wapagazi  wanaopanda Mlima Kilimanjaro wamejitolea kuzoa taka za plastiki eneo la Kwamrombo Jijini Arusha kwa lengo la kuhakikisha mazingira yanatunzwa.

Wapagazi hao zaidi ya 100 wa kampuni ya utalii ya Easy Travel And Tours Ltd walijotolea kuokota chupa za plastiki soko la Kwamrombo hadi eneo la Kona ya Mbauda Jijini Arusha.

Akishiriki katika zoezi hilo Mkurugenzi wa Jiji la Arusha,Athumani Kihamia  alisema wapagazi hao wameona umuhimu wa kutunza mazingira kwa kuokota chupa za plastiki na mifuko ya plastiki ili kuzichakata kwaajili ya kuzalisha mali ghafi.

Alisema kwakuwa eneo hilo la kwamrombo ni maarufu kwa watu kula nyama hata takataka za plastiki zinakuwa nyingi hivyo zoezi hilo ni zuri kwani hivi sasa wananchi watajua umuhimu wa kutenga taka za plastiki kwaajili ya kuzalisha bidhaa mbalimbali.

Naye Mkurugenzi wa kampuni ya Easy Travel,Musadic Husein amesema wameamua kufanya usafi katika eneo hilo kwaajili ya kutunza mazingira ikiwemo kuhakikisha taka za plastiki zinachakatwa sambamba na kuzalisha bidhaa mbalimbali za majumbani ikiwemo mbao.

Naye mmoja kati ya wafanyakazi hao,James Makoye amesema zoezi hilo liwe endelevu kwaajili ya kusaidia Jiji la Arusha kuwa safi sambamba na wananchi kujengewa utamaduni wa kuhakikisha wanatunza mazingira kwente maeneo yanayowazunguuka
Wapagazi Wajitolea kukusanya chupa za plastiki jiji la Arusha Wapagazi Wajitolea kukusanya chupa za plastiki jiji la Arusha Reviewed by KUSAGANEWS on June 03, 2018 Rating: 5

No comments: