Kiongozi wa
muungano wa upinzani wa Nasa, Raila Odinga amesema Rais John Magufuli amempa
salamu kwa ajili Rais wa nchi hiyo, Uhuru Kenyatta.
Akizungumza
leo Ijumaa Juni1, 2018 katika maadhimisho ya miaka 55 ya Madaraka Day, Odinga
amesema alipigiwa simu na Magufuli aliyempa salamu hizo, bila kueleza kwa kina
“Kwanza
nimeleta salamu kutoka kwa rafiki wa Wameru Rais jirani wa Tanzania Mheshimiwa
Magufuli, wengine mnakumbuka nilimleta Magufuli hapa wakati tunazindua ujenzi
wa barabara ya Meru leo asubuhi amenipigia simu kwamba nikifika nilete salamu
kwa Rais Uhuru,” amesema.
Katika hatua nyingine amewataka raia wa nchi
hiyo kuungana na kuacha ubaguzi na ukabila, hiyo kuangalia namna watakavyoweza
kusonga mbele kijamii na kiuchumi
Odinga ambaye
hivi karibuni amemaliza tofauti na Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amesema,
“wakenya tuungane pamoja, tuache ubaguzi, tuache ukabila na ufisadi ili tuweze
kumaliza matatizo yetu.”
“Kinamama na
vijana wapate kazi na wazee mpate malupulupu. Mimi na kijana mwenzangu Uhuru
tumeshikana pamoja na ndiyo maana mmeona leo hii tumekuwa pamoja hapa.”
Odinga apeleka salamu za Magufuli Kenya
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 01, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 01, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment