Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dk Adelardus Kilangi
amewaondoa hofu wabunge kuhusu kushtakiwa na kufilisiwa na wawekezaji wakati wa
utekelezaji wa sheria mpya za usimamizi wa madini nchini zilizofanyiwa
marekebisho mwaka jana
Akichangia bajeti ya Wizara ya Madini kwa mwaka wa fedha
2018/19, Kilangi amesema hawapaswi kuogopa kwa sababu sheria hizo zimetokana na
mikataba ya kimataifa na matamko ya Baraza la Umoja wa Mataifa
“Kuna baadhi ya watu wanasema sheria mbili zilizotungwa kuwa
tumewavunja wawekezaji, sheria hizi zimetokea wapi? Lakini zimekuwepo
kupitia Baraza la Umoja wa Mataifa na baadaye kuingia katika miktaba ya
kimataifa.” Amesema.
Amezitaja haki kuu nne muhimu ambazo zinapatikana katika
matamko ya baraza la mataifa pamoja na mikataba ya kimataifa kuwa ni haki ya
nchi kumiliki maliasili, kusimamia na kudhibiti uendelezaji wa raslimali, haki
ya nchi na watu wake kushiriki na haki ya nchi kunufaika na rasilimali zake
Mwanasheria Mkuu awatoa hofu wabunge
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 01, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 01, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment