Spika Job Ndugai amesema vita ya ufisadi aliyoianzisha Rais
John Magufuli inatakiwa kuungwa mkono na kila Mtanzania, akiwataka wanaopinga
kukaa sawa kwa kuwa mwendo ni uleule
Ametoa kauli hiyo leo Jumamosi Juni 2, 2018 katika viwanja
vya Bunge mjini Dodoma wakati akipokea taarifa mbili za kamati za Bunge
alizoziunda kuchanguza gesi asilia na uvuvi wa bahari kuu.
Amesema baadhi ya Watanzania waliandika magazetini na baadhi
ya wabunge kupinga alipounda kamati ya kuchunguza madini ya almasi na
Tanzanite, ripoti zake kuwaislishwa serikalini
Amebainisha kuwa matokeo ya kamati hizo yameanza kuonekana,
ikiwamo mauzo ya madini ya Tanzanite kupanda huku akigusia jinsi ukuta
kuzunguka mgodi huo ulivyojengwa
“Kama tungekuwa sawa tusingekuwa hapa tulipo na nimpongeze
Rais wetu, jambo hili si jepesi hapa tunashughulika na majitu yenye fedha
nyingi, yamebaki kutununua nua tu,” amesema Spika Ndugai
“Tumempata kiongozi, katika Ikulu yake hakuna hata mmoja
anayekanyanga, lazima tumuunge mkono na wale wanaotupinga wakae sawa ila mwendo
ni huo huo.”
Kuhusu mikataba, Nduigai amesema hiyo ndio yenye shida
zaidi, “mikataba imetuumiza sana, hii kampuni ya Songas ni ya
kinyonyaji, kupitia mikataba ya hovyo wameitishwa Tanesco mizigo ya ajabu
kwa kushirikiana na kampuni ya PAP. Kampuni hizi zimeiumiza sana TPDC (Shirika
la Maendeleo ya Petroli Tanzania) kwa kuitishwa masharti ya ajabu ikiwamo
kuibebesha gharama za uendeshaji.”
Akizungumzia utaratibu huo wa Bunge kuunda kamati za
uchunguzi na taarifa kuwasilishwa serikalini amesema kila uongozi ana
utaratibu wake na huo anaoufanya yeye anaona unafaa
“Sisi tunafanya kazi yetu, tunakuja katika umma tunawasilisha
taarifa zetu, kwa hiyo tuwapuuze watu hawa kwani hawana nia njema,” amesema
Ndugai ataka Magufuli kuungwa mkono vita dhidi ya ufisadi
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 02, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 02, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment