Mke wa Bilionea Msuya ataka tume ya uchunguzi


Mke wa marehemu bilionea, Erasto Msuya, Miriam Mrita ameiomba  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuunda tume kuichunguza kwa kina kesi ya mauaji inayomkabili akidai kuna uonevu unaoendelea

Miriam amewasilisha ombi hilo leo Juni 4 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba mara baada ya wakili wa serikali, Patrick Mwita kuiambia mahakama kuwa kesi ilipangwa kwa ajili ya kutajwa, lakini  jalada halisi lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) na kuomba ipangiwe tarehe nyingine ya kutajwa

Baada ya Mwita kueleza hayo, Miriam alinyoosha mkono ambapo hakimu Simba alimruhusu kuongea

Miriam alisimama na kuiambia mahakama kuwa huu ni mwaka wa pili sasa wanaendelea kusota mahabusu.

 "Mimi ni mama mjane, mume wangu ameuawa, mimi nipo mahabusu gerezani kwa miaka miwili, kama mama sijui watoto wangu wanaendeĺeaje huko nje." Ameongea Miriam

Ameongeza kuwa amechoshwa na wimbo wa upande wa mashtaka kuwa upelelezi bado haujakamilika

"Mtu ukishafiwa na mume kuna vurugu mechi zinaendelea huko nje, naomba iundwe tume ya uchunguzi wa kina ya kuichunguza kesi hii kwa sababu kuna uonevu ambao unaendelea."Ameeleza Mrita

Amebainisha mahakamani hapo kuwa kesi yake ipo kifamilia zaidi na kuomba iangaliwe zaidi na kwamba watagundua mambo mengi zaidi
Anadaiwa kumuua kwa makusudi dada  wa marehemu bilionea Erasto Msuya, Anathe Msuya Mei 25, 2016 huko Kibada Kigamboni Jijini Dar es Salaam.
Mke wa Bilionea Msuya ataka tume ya uchunguzi Mke wa Bilionea Msuya ataka tume ya uchunguzi Reviewed by KUSAGANEWS on June 04, 2018 Rating: 5

No comments: