Rais John
Magufuli amewataka watendaji kutoa taarifa za masuala ya kilimo kabla
hawajasemwa
Ametoa maagizo
hayo leo Juni 4 alipokuwa akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa awamu ya pili
ya programu ya kuendeleza kilimo
Amesema
wamekuwa wakifanya juhudi mbalimbali kuboresha sekta ya kilimo ikiwamo kutafuta
fedha kwa ajili ya kuiendeleza, lakini kuna wanaosema hazitengwi fedha kwa
ajili ya sekta hiyo
“Tunapeleka
lakini inawezekana hazitoshi, wengi wanaosema hatupeleki wanaangalia sekta ya
kilimo kwa upekee na kusahau baadhi ya fedha za kilimo zipo kwenye wizara ya
maji, nishati, mifugo na uvuvi, Wakala wa Barabara Vijijini (Tarura) na
ardhi, ”amesema
Amesema
wanasemwa kwa sababu waliopo serikalini hawasemi mambo kama hayo, badala yake
wamekaa kimya na hawatoi taarifa za ukweli katika hayo wanayosemwa
“Tusikae kimya
tukaendelea kusemwa, tukifanya hivi yale tunayosemwa yataonekana ya ukweli,
niwaombe sana viongozi wenzangu wote hadi wakuu wa mikoa masuala mbalimbali ya
kilimo yanapoulizwa tuwe tunatoa majibu na ikiwezekana tuyatoe kabla ya
kusemwa,” amesema Dk Magufuli.
JPM: Watendaji tuseme kwa uwazi yanayohusu kilimo
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 04, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 04, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment