Rais John
Magufuli amesema hajaridhika na utendaji kazi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo
(TADB).
Akizungumza
leo Juni 4 katika hafla ya uzinduzi wa Awamu ya pili ya Programu ya
Kuendeleza Kilimo (ASDP II) Rais Magufuli amesema hafahamu kama
mkurugenzi wa benki hiyo yupo ofisini na anafanya kazi
Amesema
Serikali iliipa mtaji wa Sh60bilioni TADB, mwaka 2017 baada ya
kukopa zaidi ya Sh207.05 bilioni kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa
ajili ya kuiongezea mtaji benki hiyo
Amesema
tayari benki hiyo imeshatoa awamu ya kwanza ya mkopo huo ambayo ni
Sh102.7 bilioni lakini bado utoaji wa mikopo kwa wakulima umekuwa ni wa
kusuasua badala yake wamejikita kufanya biashara na benki nyingine
Magufuli
amesema Serikali inakopa wakakopeshwe wakulima lakini benki hiyo inachukua
fedha hizo na kwenda kufanya biashara na benki nyingine
Amesema
kuanzia Januari hadi Desemba, 2017, benki hiyo ilifanya biashara na benki
nyingine kwa kiasi cha Sh 82.3bilioni
“Ina maana
wakulima kwa mwaka huo hawajapata mkopo wowote kwenye benki ya Serikali,
sifahamu kama mkurugenzi huyo bado yupo anafanya kazi
“Hili ni suala
la wizara ya fedha, suala la benki kuu, hamuwezi, wakulima wanahangaika
hawakopeshwi fedha zao,” amesema Magufuli.
JPM haridhishwi na mwenendo wa Benki ya Kilimo
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 04, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 04, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment