Mbunge wa
Mtambile (CUF), Masoud Abdallah Salim ameibuka na kuibana serikali kuwa ni lini
itaanza kutumia teknolojia ya kisasa ya mate katika kutambua waathirika wa
Virusi Vya UKIMWI kama wanavyofanya nchi nyingine duniani na kuachana na ile ya
kutoa damu.
Mbunge Masoud ametoa kauli hiyo Bungeni Jijini Dodoma
Mei 31, 2018 wakati alipokuwa anauliza swali la nyongeza kuwa hali ya
maambukizi ya virusi vya UKIMWI katika Jiji la Dodoma yanaongezeka kwa kasi
ambalo alikuwa amelielekeza kwenye Wizara ya Afya.
Akijibu
swali hilo, Waziri Ummy Mwalimu amekiri kuwepo kwa ongezeko la maambukizi
ya VVU ambapo yamepanda kuanzia mwaka 2012 hadi 2017 na katika mkoa wa Dodoma
maambukizi yameongezeka kutoka asilimia 2.4 hadi tano sawa na mikoa ya Tanga na
Mwanza na wanafanya utafiti maalum ili kubaini sababu za
"Ni
kweli tumekuwa na changamoto ya watu kuwapata kupima hasa wanaume na tumeona
njia ambayo itaweza kusaidia wanaume kupima Ukimwi ni njia ya mtu kujipima
mwenyewe. Kwa sasa sheria iliyopo imekuwa kikwazo kutimiza hilo, hivyo
wataandika barua kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) ili kuwasilisha muswada
wa mabadiliko ya sheria ambayo pamoja na mambo mengine, itaruhusu mtu kujipima
VVU ikiwamo kwa njia ya mate ili ndani ya dakika 15 apate majibu", amesema Ummy.
Pamoja na
hayo, Ummy Mwalimu ameendelea kwa kusema "tunaamini mtu akijipima na
kujua majibu itakuwa kichocheo cha kwenda katika kituo cha afya ili kuthibitika
na kuingizwa kwenye mpango wa dawa. Nasisitiza dawa za kufubaza virusi vya
UKIMWI (ARV) zipo kwa asilimia 100, watu wapime Ukimwi tena si kifo".
Kwa upande
wake, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira,
Anthony Mavunde amesema serikali imeridhia mkakati wa Shirika la Afya Duniani
(WHO) wa kupima VVU na kutibu bila kuzingatia kiwango cha kinda mwilini (CD4).
a
Mbunge ataka serikali itumie kipimo cha mate
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 01, 2018
Rating: 5
No comments:
Post a Comment