Malezi ya Maria na Consolata, yalisimamiwa na Mungu

Mkuu wa Shirika la Masista la Maria Consolata, Jane Nugi alisema malezi ya pacha walioungana, Maria na Consolata Mwakikuti, yamesimamiwa na Mungu

Akizungumza leo Juni 6 wakati wa ibada ya mazishi yao, Ngugi amesema tangu walipozaliwa wamepita katika mikono ya watu wengi waliochangia ndoto zao kufikiwa

Amesema waliwalea kwenye misingi ya kumcha Mungu, kujiamini na kuona kuwa hakuna kigumu mbele yao

Huku akiwatambulisha wengine walioshiriki kwenye malezi ya pacha hao

“Baada ya kuzaliwa tuliamua kuwapa majina ya Maria na Consolata kutokana na namna walivyozaliwa,” amesema

Akitoa salam za familia ya Mshumbusi, Mjomba wa Maria na Consolata, Elisha Mshumbusi amesema kuna wakati walitoweka kwenye malezi ya mapacha hao lakini Masister wa Shirika la Maria Consolata na Albetina Mbilinyi waliwasaidia

Amesema japo walikuwa na ulemavu lakini pacha hao walijaa tabasamu usoni na moyoni

"Ni pigo lakini tunalo la kujifunza, asante sana kila aliyeshiriki kwa namna moja au nyingine kwa malezi yao mapacha wetu," amesema Mshumbusi.
Malezi ya Maria na Consolata, yalisimamiwa na Mungu Malezi ya Maria na Consolata, yalisimamiwa na Mungu Reviewed by KUSAGANEWS on June 06, 2018 Rating: 5

No comments: