Mahakama yamuachia huru mmiliki Jamii Forum


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaachia huru Mkurugenzi Mtendaji wa mtandao wa Jamii Forums, MaxenceMelo na Mwanahisa wa  mtandao huo, Micke William baada ya kuwaona hawana kesi ya kujibu

Hakimu Mkazi Mwandamizi, Godfrey Mwambapa aliwaachia huru washtakiwa hao leo Juni 1, baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na mashahidi sita wa upande wa mashtaka na kuona ushahidi huo hauna mashiko

“Hakukuwa na ushahidi unaoeleza moja kwa moja wa barua hiyo ya kuwataka watoe taarifa za kampuni yao na ushahidi huo una mashaka?” amesema Mwambapa

Katika kesi hiyo Melo na mwenzake wanadaiwa kuzuia uchunguzi wa jeshi la polisi kwa kukataa kutoa taarifa za kampuni yao

Awali, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa,amedai kuwa baada ya usajili, kampuni hupewa taarifa za siri ambazo huwezesha mtu kuingia katika mtandao huo husika hivyo washtakiwa hao walikuwa na uwezo kuona taarifa kwenye mfumo wao

Kishenyi amedai kuwa kufuatia jitihada hizo za Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalum(ZCO) za kuwataka washtakiwa kutoa taarifa muhimu na wao kukataa walikamatwa na kufikishwa mahakamani

Mahakama yamuachia huru mmiliki Jamii Forum Mahakama yamuachia huru mmiliki Jamii Forum Reviewed by KUSAGANEWS on June 01, 2018 Rating: 5

No comments: