Mbunge wa Iringa mjini
(CHADEMA) mchungaji Peter Msigwa, amesema kuwa wakazi wa Mkoa wa Kigoma
wamesahaulika na Serikali ni kama wapo nje ya Tanzania kutokana na ubovu
wa barabara ya Nyakanazi
Msigwa
amesema hayo leo Juni 4, 2018 Bungeni Jijini Dodoma wakati wa kuchangia
hoja mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Fedha na
Mipango katika mwaka wa Fedha 2018/2019 na kudai kuwa wabunge wanapaswa
kuungana pamoja kuishinikiza Serikali ijenge barabara hiyo.
“Kuhusiana na barabara ya Nyakanazi, tangu nimekuwa
Mbunge kipindi cha kwanza nimekuwa nikisikia Kigoma Nyakanazi, kwakweli
watu wa Kigoma mnaonewa inabidi tuwasaidie, mpigiwe debe kwakweli mpo
porini sana mmetengwa, mimi ilikuwa mara ya kwanza kufika Kigoma
kwakweli mpo nje ya Tanzania” amesema Msigwa.
Kwa upande mwingine Mbunge huyo amesema kuwa Wizara ya Fedha na
Mipango imejikita zaidi katika masuala ya fedha na kusahau kujihusisha
na mipango kwasababu mipango mingi inayotekelezwa ipo nje ya mpango wa
miaka mitano wa Taifa hivyo kushindwa kutekeleza vipaumbele vya
maendeleo ya nchi.
Leo Juni 4, 2018 Bunge linajadili Bajeti ya Wizara ya Fedha na
Mipango katika mwaka wa fedha 2018/2019 na Waziri husika Dkt. Philip
Mpango ameomba Bunge kuizinisha jumla shilingi trilioni 12.5 ambapo
trilioni 10.07 ni katika matumizi ya kawaida na shilingi trilioni 1.2
kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.
“Kigoma mpo nje ya Tanzania”- Msigwa
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 04, 2018
Rating: 5
No comments:
Post a Comment