Mbunge wa Momba (Chadema), David Salinde amesema Wizara ya
Fedha na Mipango ndio adui namba moja wa maendeleo ya Taifa na kushauri Bunge
liichukulie hatua ili kutekeleza maagizo yake
Silinde akichangia bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango ya
mwaka 2018/19, leo Juni 4, 2018 bungeni, amesema: “Kwa lugha nyepesi kabisa,
adui namba moja ni Wizara ya Fedha na Mipango. Wizara ya fedha inashindwa kutoa
fedha ambazo zipo kisheria.”
Silinde amesema ukiangalia ripoti za CAG, wizara imekusanya
fedha lakini haipeleki sehemu husika
“Leo watu wa korosho wanalalamika wamekusanya Sh91 bilioni,
wamepelekewa Sh10 bilioni,”amesema
Ameongeza: “Wana sababu moja tu, uhakiki na ndio kichaka cha
kujifichia kupeleka fedha. Mawaziri wanakuja hapa wanalia. Wao wajibu wao
kukusanya na kupeleka. Hivi hawa wanaitakia mema nchi hii”
Kesho mpo ninyi, atakuja Rais wa awamu wa sita, Rais
hashtakiwi, tutawachukulia hatua ninyi mawaziri.”
David Silinde: Wizara ya Fedha adui namba moja wa maendeleo
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 04, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 04, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment