Basi lagonga treni, saba wafariki

Watu saba wamekufa na wengine 20 kujeruhiwa leo saa 12 asubuhi baada ya basi walilopanda kugonga treni ya mizigo eneo la Gungu mkoani Kigoma

Akiongea Kamanda wa polisi mkoani humo, Martin Otieno amesema chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa basi la Prince Amida kutozingatia alama za barabarani

“Ni kweli ajali imetokea leo asubuhi. Tupo eneo la tukio hapa kwa taarifa za awali watu saba wamefariki hadi sasa na wengine ishirini kujeruhiwa ila bado tunaendelea kuokoa miili mingine tutatoa taarifa zaidi baadae,” amesema Otieno

Otieno amesema dereva wa basi hilo ambalo hufanya safari zake kati ya Kigoma kwenda Nzega mkoani Tabora amefariki  na mkono mmoja umekatika


Basi lagonga treni, saba wafariki Basi lagonga treni, saba wafariki Reviewed by KUSAGANEWS on June 06, 2018 Rating: 5

No comments: