Baraza Kuu la
Waislamu Tanzania (Bakwata) limewatoa hofu waislamu wanaotarajia kwenda kwenye
ibada ya hijja, likieleza kuwa limejipanga vyema kuhakikisha upungufu
uliojitokeza mwaka jana haujirudii
“Taasisi nne
ambazo ni Tanzania Chartable Oraganization, Haji Khikma, Taquwa Haji Group na
Almadina Social Services Trust hazitosafirisha mahujaji kwa kuwa hazijakidhi
masharti yaliyowekwa. Hatutaki mambo yaliyojitokeza mwaka jana, yajirudie
sasa,” amesema Sheikh Hamisi Mataka, mwenyekiti wa baraza hilo.
Mataka ametoa
kauli hiyo leo Jumamosi Juni 2, 2018 jijini hapa, katika mkutano wake na
waandishi wa habari, kubainisha kuwa zaidi ya mahujaji 100 mwaka, 2017
walikwama kwenda kufanya ibada hiyo baada ya taasisi ya Twaiba iliyokusanya
fedha zao kwa madai ya kuwawezesha kusafiri, kuingia mitini.
“Mpaka sasa mambo yote yanakwenda vizuri,
hakuna tishio lolote ambalo tumelibani la mahujaji kutosafiri kwa sababu mambo
yote yapo katika mstari kuhakikisha kuwa waislamu wanatekeleza ibada
hiyo,”amesema Mataka
Mataka amesema
moja ya hatua walizozichukua ni pamoja na kutoruhusu taasisi zisizokidhi vigezo
kuwadanganya tena wananchi
Mataka alisema
taasisi 11 pekee ndizo zilizokidhi vigezo na msharti yaliyowekwa ikiwemo ,
Alhusna Haji Trust, Shamsul Maarifa Kheri na Tanzania Muslim Development
Asociatiaon, Tanzania Muslim Haji Trust
Katika hatua
nyingine Mataka amessema kuanzia Juni 8, 2018 waislamu nchini kupitia misikiti
yao watafanya harambee ya kuchangia maendeleo ya baraza hilo ili liweze
kutekeleza majukumu yake mbalimbali, ikiwemo kuwalipa watumishi.
Bakwata yazipiga ‘pini’ taasisi nne kujihusisha na ibada ya hijja
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 02, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 02, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment