Baraza la Madiwani lamsimamisha kazi meneja Suwasa


Baraza la Madiwani la halmashauri ya wilaya ya Sikonge mkoani Tabora limemsimamisha kazi Meneja wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (SUWASA) wilayani humo, Benjamini Brighton Mujuni kwa tuhuma mbalimbali ikiwemo matumizi mabaya ya fedha za mradi wa maji

Uamuzi wa kusimamishwa kazi mtendaji huyo umetangazwa leo Mei 27 na mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo, Peter Nzalalila, baada ya kufanyika kikao cha baraza la madiwani juzi Jumamosi, Mjini Sikonge

Nzalalila amesema madiwani wamejadili kwa kina tuhuma mbalimbali zinazomkabili na kujiridhisha pasipo shaka kuwa meneja huyo, ameenda kinyume na maadili ya utumishi wa umma

“Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais John Magufuli haitaki kusikia ubadhirifu au uzembe wa aina yoyote ile kwa mtendaji au mtumishi wa umma, na hii ni salamu kwa kila mtumishi kutekeleza wajibu wake ipasavyo vinginevyo tutamwondoa,”alisema

Mwenyekiti wa Bodi ya Suwasa, Juma Ikombola, alisema walipokea barua za malalamiko ya kunyanyaswa wafanyakazi wake ikiwemo kutopeleka makato yao ya NSSF benki, kwa kipindi cha mwaka mzima sasa.
Baraza la Madiwani lamsimamisha kazi meneja Suwasa Baraza la Madiwani lamsimamisha kazi meneja Suwasa Reviewed by KUSAGANEWS on May 27, 2018 Rating: 5

No comments: