Tetemeko la ardhi lililodumu kwa takribani
dakika moja usiku wa kuamkia leo Machi 25, 2018 limetokea Mkoa wa Mwanza,
Kagera na Geita, kuzua taharuki kwa wakazi wa mikoa hiyo, huku
baadhi wakijaribu kukimbia nyumba zao kwa nia ya kujiokoa
Hata hivyo hakuna madhara ya vifo au
uharibifu ulioripotiwa hadi jana
Jiolojia Mwanandamizi kutoka Wakala wa
Jiolojia Tanzania (GST), Gabriel Mbogomi amesema tetemeko hilo lina ukubwa wa
richa 4.6 na lilikuwa likitokea Kaskazini Magharibi ya Mji wa Kahama kuelekea
kusikojulikana
Kwa mujibu wa GST, Tanzania ni miongoni mwa
nchi zinazotokewa na tetemeko la ardhi kutokana na kuwa sehemu ya mkondo wa
Bonde la Ufa.
Tetemeko la ardhi latikisa Kagera,Mwanza
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 25, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment