Rais John Magufuli leo Jumapili Machi 25
amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evaristi Ndikilo
kufuati ajali iliyotokea na kusababishsa vifo vya watu 26.
Ajali hiyo iliyotokea saa tatu usiku ilihusisha gari aina ya Hiace iliyokuwa imebeba abiria kugongana na lori lililokuwa limebeba chumvi katika Kijiji cha Mparange Wilaya ya Mkuranga Mkoa wa Pwani
“Nimesikitishwa sana na taarifa ya vifo vya
watu 26 waliopoteza maisha kwenye ajali ya barabarani iliyotokea huko Mkuranga
mkoani Pwani, tumepoteza idadi kubwa ya Watanzania wenzetu na nguvu kazi ya
Taifa,” amesema Rais Magufuli
Rais katika salamu za rambirambi alizotoa
amemtaka Mhandisi Ndikilo kumfikishia salamu za pole kwa familia za marehemu
ndugu jamaa na marafiki na wote walioguswa na vifo hivyo pamoja na kuvitaka
vyombo vya usalama kushughulikia usalama wa barabarani na kuchunguza ajali hiyo
pamoja na kuchuku hatua stahiki
“Naungana na wafiwa wote katika kipindi hiki
kigumu cha majonzi ya kuondokewa na wapendwa wao na watu aliowategemea,”amesema
Rais Magufuli
Amewaombea marehemu wote wapumzike mahali pema peponi na majeruhi tisa wa ajali hiyo wapone haraka ili waungane na familia na jamaa zao katika shughuli zao za kila siku
Basi hilo lilikuwa likitokea Mkuranga
kuelekea Kimanzichana wakati lori lilikuwa likitoka Lindi kuelekea Dar es
Salaam.
Rais Magufuli atuma salamu za rambirambi Mkuranga kufuatia ajali iliyouwa watu 26
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 25, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment