Serikali imesema wanafunzi wa vyuo vikuu
wanaongoza kutukana na kutumia lugha zisizo na maadili kwenye mitandao ya
kijamii.
Angalizo hilo limetolewa na naibu waziri wa
Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha jana Jumamosi Machi 24,
2018 katika hafla fupi ya uzinduzi wa Unilife Compus iliyopo Mkoa wa
Kilimanjaro uliofanyika katika Chuo Kikuu cha Mwenge na kuvikutanisha vyuo
vikuu vyote vya mkoa huo.
Amesema yapo mambo matatu ambayo
yanachangia wanafunzi kutofanya vizuri, yakiwamo matumizi mabaya ya Teknolojia
ya Habari na Mawasiliano (Tehama), anasa na starehe zilizopitiliza na
kujiingiza kwenye siasa ambazo zinawanyima fursa ya kusoma vizuri
“Serikali imebaini mambo yanayochangia
kufifisha na kudidimiza jitihada za elimu tunayoitoa kuonekana bure. Kuna vitu
ambavyo siyo vizuri vinaendelea katika vyuo vyetu, ndizo changamoto
tunatakiwa kukabiliana nazo. Chuoni unaweza kutengeneza au kuharibu maisha
yako,” amesema.
Naye mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira amesema wanafunzi wengi hawataki kujifunza kwa kutumia muda vizuri kwa kusoma vitabu
"Tunabaki kuwa waigaji wa dhana za
wenzetu wa magharibi, hatutaki kujifunza vitu vipya bali vilevile vya wenzetu
vinatumika hadi leo. Wasomi wa Tanzania tunajishusha kwa sababu ya kushindwa
kuleta mawazo mapya kwenye sekta ya elimu na afya," amesema Mghwira
SERIKALI YASEMA WANAFUNZI WA VYUO WANAONGOZA KWA LUGHA ZA MATUSI MITANDAONI
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 25, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment