Lissu afanya mkutano Jimboni Kwake kwa kutumia Video Call kutoka Ubelgiji


Mbunge wa Singida Mashariki ambaye yupo Ubelgiji akipata matibabu, Tundu Lissu, amefanya mkutano wa “Video Call” na Wajumbe wa Kamati Tendaji na Madiwani wa Jimbo lake,
Lissu aliwaambia madiwani na viongozi wake maendeleo ya afya yake na kuwasisitizia kutokubali kughiribiwa.

“Kwa kweli, ninaendelea vizuri. Afya yangu inazidi kuimarika. Nawahakikishia, nitarudi nikiwa mzima na ninayetembea." alisema Lissu

"Ninawaamini sana. Sina mashaka yeyote na ninyi. Naomba pigeni kazi ili kulinda heshima yenu na hadhi zenu mlizopewa na wananchi."

Mkutano huo pia ulihudhuriwa na Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea ambaye aliombwa na Lissu kukutana na wajumbe hao,
Katika mkutano huo uliofanyika mjini Ikungi, Kubenea aliongozana na Mwenyekiti wa Chadema, Kanda ya Kati, Alphonce Mbasa; katibu wa Kanda, Iddi Kizota na mbunge wa Viti Maalum, mkoani Singida, Jessica Kishoa.

Kubenea na viongozi wenzake waliwaeleza madiwani na viongozi hao wa kata kuwa wanalo jukumu kubwa la kukilinda chama na kumtetea mbunge wao kwa gharama yeyote ile.

Lissu afanya mkutano Jimboni Kwake kwa kutumia Video Call kutoka Ubelgiji Lissu afanya mkutano Jimboni Kwake kwa kutumia  Video Call kutoka Ubelgiji Reviewed by KUSAGANEWS on March 25, 2018 Rating: 5

No comments: