Mbunge wa Singida Mashariki ambaye
yupo Ubelgiji akipata matibabu, Tundu Lissu, amefanya mkutano wa “Video Call”
na Wajumbe wa Kamati Tendaji na Madiwani wa Jimbo lake,
Lissu aliwaambia
madiwani na viongozi wake maendeleo ya afya yake na kuwasisitizia kutokubali
kughiribiwa.
“Kwa kweli, ninaendelea vizuri. Afya yangu inazidi kuimarika. Nawahakikishia, nitarudi nikiwa mzima na ninayetembea." alisema Lissu
"Ninawaamini sana.
Sina mashaka yeyote na ninyi. Naomba pigeni kazi ili kulinda heshima yenu na
hadhi zenu mlizopewa na wananchi."
Mkutano huo pia
ulihudhuriwa na Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea ambaye aliombwa na Lissu
kukutana na wajumbe hao,
Katika mkutano huo
uliofanyika mjini Ikungi, Kubenea aliongozana na Mwenyekiti wa Chadema, Kanda
ya Kati, Alphonce Mbasa; katibu wa Kanda, Iddi Kizota na mbunge wa Viti Maalum,
mkoani Singida, Jessica Kishoa.
Kubenea na viongozi
wenzake waliwaeleza madiwani na viongozi hao wa kata kuwa wanalo jukumu kubwa
la kukilinda chama na kumtetea mbunge wao kwa gharama yeyote ile.
Lissu afanya mkutano Jimboni Kwake kwa kutumia Video Call kutoka Ubelgiji
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 25, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment