Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amewataka
wafanyabiashara wilayani hapa kutumia taasisi za fedha kukopa kwa ajili ya
kukuza mitaji yao
Ameyasema hayo leo Jumapili Machi 25,
2018 wakati akizungumza na wafanyabiashara wa wilaya hiyo katika kikao
kilichofanyika ukumbi wa Chama Cha Walimu (CWT) Ruangwa
Waziri Mkuu ambaye yuko wilayani Ruangwa kwa
ziara ya kikazi ya siku mbili, amesema ni vyema wakatumia taasisi za fedha
zilizopo ili kukuza mitaji yao
”Naamini sekta ya biashara ni muhimu katika
mabadiliko ya maendeleo, hivyo wafanyabiashara ni chachu ya maendeleo kokote na
Serikali itaendelea kuwaunga mkono.” Amesema
Amesema katika kuhakikisha riba zinapungua,
Rais John Magufuli anaendelea kuzungumza na wamiliki wa taasisi za fedha
ili waone namna ya kupunguza riba hizo
Naye mwenyekiti wa Umoja wa Wafanyabiashara Wilaya
ya Ruangwa, Said Shea amewaomba wenzake kutumia fursa za maendeleo
zilizopo wilayani humo kwa kupanua wigo wa biashara zao.
Majaliwa awataka wafanyabiashara kukopa
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 25, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment