Baada ya utafiti kubaini mwamko mdogo kwa
wanaume kupima nakutumia dawa za kufubaza makali ya Virusi
vya Ukimwi (ARVs), Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (Tacaids) sasa
kuanzisha kampeni maalumu
kizungumza leo Jumapili Machi 25, 2018 na
Kamati ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi na Kupambana na Dawa za Kulevya,
mkurugenzi mkuu Tacaids, Dk Leonard Maboko amesema kampeni hiyo itakuwa
miongoni mwa shughuli zitakazofanywa katika mkakati wa nne wa kupambana na
Ukimwi nchini
“Katika utafiti wa mwaka 2016/17,
tuliangalia vitu vipya ambavyo ni maambukizi mapya na kiwango cha kufubaza
VVU.
Tuligundua ingawa wanawake wanaongoza katika
maambukizi mapya, lakini ni wepesi kupima na kutumia dawa kikamilifu ndiyo
maana kwenye kiwango cha kufubaza wanaongoza,”amesema
Amesema katika utafiti huo uliozinduliwa
Desemba mwaka jana, kiwango cha watu kufubaza VVU kwa wenye miaka kati
ya 15 na 64 ni asilimia 52 lakini kati ya hao, 57.5 ni wanawake na wanaume ni
41.2
Amesema kwa mujibu wa Mkakati wa Taifa wa
Ukimwi unaoishia mwaka huu gharama za kugharamia Ukimwi nchini zinakadiriwa
kufikia Sh6 trilioni kwa muda wa miaka mitano
Naye waziri wa nchi katika Ofisi ya Waziri
Mkuu (Sera), Jenista Mhagama amesema mwaka 2015 wafadhili wa tume hiyo walianza
kupunguza fedha za mapambano dhidi ya VVU.
Kampeni ya kupima Ukimwi wanaume yaja
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 25, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment