Mahakama ya Hakimu
Mkazi Iringa imetoa dhamana kwa Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi nchini Abdul
Nondo nchini aliyekuwa akishikiliwa na jeshi la polisi tangu Machi 7 Mwaka huu.
Kupitia Wakili wa
Mwenyekiti huyo ambaye pia ni Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Jebra
Kambole amesema kuwa Mahakama hiyo imetoa dhamana kwa masharti ya wadhamini
wawili mmoja awe mtumishi wa serikali, wote wawe wakazi wa Iringa.
Aidha ameongeza kuwa
mbali na masharti hayo Wadhamini wanapaswa kusaini bondi ya kauli Tshs Mil
5.
Kesi ya Abdul Nondo
itarudi tena mahakamani hapo Aprili 10, 2018.
Nondo anashtakiwa kwa
makosa mawili ambapo kosa la kwanza ni kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni
kuwa yupo hatarini akiwa katika eneo la Ubungo na kuzisambaza kwenye mtandao wa
Whatsapp na kosa la pili limetajwa kuwa ni kutoa taarifa za uongo kwa mtumishi
wa umma Mafinga wakati alipokuwa akitoa taarifa katika kituo cha polisi mjini
humo kwa kusema kuwa alitekwa na watu wasiojulikana
Abdul Nondo apata Dhamana
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 26, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment