Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)
kimesema kimepata pigo baada ya kuondokewa na mmoja wa waasisi wake, Victor
Kimesera.
Amesema Chadema kimempoteza mmoja wa watu wake muhimu waliokuwa nguzo ya ustawi wa chama hicho
“Mzee Kimesera amekuwa katikati ya mapambano, tangu aliposhiriki kuasisi chama hiki, hadi mauti yalipomkuta akiwa mtendaji wa chama makao makuu. Tumepokea msiba huu kwa mshtuko mkubwa sana,” amesema
“Mzee Kimesera maarufu 'VPK' kama
tulivyozoea kumuita, ametutoka kipindi ambacho mchango wake ungehitajika sana
hasa wakati huu ambako taifa letu linapitia katika mkwamo mkubwa wa kisiasa,”
amesema
Mbowe amesema Kimesera atakumbukwa zaidi kwa
namna alivyojitolea kwa hali na mali kupigania haki, demokrasia na maendeleo
nchini hususan katika Jimbo la Kiteto mkoani Manyara
Amesema kwa sasa Chadema kupitia ofisi ya
katibu mkuu, inashirikiana na familia ya marehemu kupanga taratibu za mazishi
“Taarifa nyingine ikiwAmo ratiba ya
mazishi yanayotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam, zitaendelea kutolewa,”
amesema
Mbowe asema kifo cha Kimesera kimeleta pigo ndani ya Chadema
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 25, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment