Naibu Katibu Mkuu Wizara
ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Avemaria Semakafu amefunguka na kuweka
wazi utata ulioibuka kuhusu kigezo cha umri wa kujiunga na masomo ya kidato cha
tano na sita na kusema taarifa ambayo inasambaa imekuwa na makosa.
Semakafu amesema kuwa yametokea
makosa ya kiuandishi ila kujiunga na masomo ya kidato cha tano na sita ni miaka
25 na siyo miaka 20 kama ambavyo inasomekana katika taarifa aliyotolewa mapema
leo.
"Kumetokea makosa ya kiandishi,
miaka ni 25 ya kujiunga sekondari na sio 20 kama ambavyo inasomeka kwenye ile
karatasi" alisema
Semakafu
Serikali yakiri kujichanganya suala la umri
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 23, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment