Jeshi la Polisi Nchini
leo Machi 22, 2018 limetoa amri ya kukamatwa kwa Mbunge wa Kawe Mhe. Halima
Mdee pamoja na Mbunge wa jimbo la Tarime, Esther Matiko kwa kile
kilichoelezwa kushindwa kuitikia wito wa jeshi la polisi.
Taarifa iliyotolewa na CHADEMA
imesema kuwa jeshi la polisi limeagiza wabunge hao wakamatwe popote walipo na
kufikishwa kituoni kutokana na kushindwa kufika katika wito huo leo.
Aidha viongozi wa CHADEMA akiwemo
Mwenyekiti wa Chama hicho Mhe. Freeman Mbowe, Katibu Mkuu wa Chama hicho Dkt.
Mashinji na Salum Mwalim ambao walifika polisi kuitika wito huo mapema leo
waliachiwa majira ya mchana wakiwa hawajahojiwa kitu chochote na kuambiwa
warudi tena Jumanne 27, 2018.
Mbali na hilo jeshi la polisi
liliendelea kuwashikilia Mbunge John Mnyika na John Heche ambao walibaki
kituoni hapo na kufanyiwa mahojiano na kisha baadae kuruhusiwa kuondoka.
Polisi yatoa amri kukamatwa kwa Halima Mdee na Ester Matiko
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 22, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment