MSTAHIKI Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya
Mwita amezitaka halmashauri zote jijini hapa kuajiri
watumishi ambao watakuwa wanafanya kazi ya kuzika miili ya watu ambao
watabainika kuwahawana ndugu.
Meya Mwita ametoa kauli hiyo jijini hapa leo kwenye
kikao cha robo ya pili ya Baraza la Madiwani wa Jiji la Dar es Salaam ,ambapo
amewaeleza madiwani hao kuwa jukumu la kuzika marehemu wasiokuwa ndugu
ni la jiji,kwakushirikiana na halmashauri hivyo wanapaswa kuwajibika katika
hilo.
Amefafanua kuwa hadi sasa jiji limeshanunua gari pamoja
na mahitaji mengine ya kuhifadhia miili hiyo pindi inatokea na kwamba
changamoto iliyopo ni watu ambao watashirikiana kutekeleza jukumu hilo.
“ Mtakuabliana na mimi kwamba tulishakubaliana
kwamba jambo hili lifanyike kwenye halmashauri zetu, lakini hadi
sasa Kinondoni pekee ndio wametimiza agizo hili, sasa ninaagiza tena
halmashauri nyingine za jiji hili kuajiri watu hao” amesema Meya Mwita.
Mwita amesema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam
pamoja na halmashauri nyingine zilizopo jijini hapo walikubaliana kuzika watu
wasiokuwa na ndugu hivyo kila mmoja anapaswa kutekeleza makubaliano hayo.
"Hivyo marehemu wanapokuwa wamekaa muda mrefu
wanalazimika kuzikwa na jiji, natulikubali kuchangia usafiri,dawa na
sanda," amesema.
Amefafanua kuwa watu wasiokuwa na ndugu
wanapokufa, wanapokaa hospitalini zaidi ya siku 20,jiji linalazimika
kuwazika hivyo wapo ambao wanazikwa kwenye halmashauri mbalimbali.
Hivyo wakati Jiji la Dar es Salaam likitimiza wajibu
wake katika kuzika marehu hao kila halmashauri linajukumu la kutoa
watumishi kwa ajili ya kuzika.
Amefafanua taarifa alizonazo ni Halmashauri ya Kinondoni
pekee ndio ambayo imeajiri watumishi kwa ajili ya kuzika miili ya watu ambao
wamefariki na hawana ndugu.
"Ni wajibu wa halmashauri kuhakikisha wanafanikisha
kupatikana kwa watumishi hao haraka," amesema Meya Mwita.
MWISHO
Imetolewa leo Machi 22 na Christina Mwagala,Afisa Habari
Ofisi ya Meya wa jiji.
Meya wa jiji la Dar awatangazia Neema Wanaozika watu wasio na ndugu
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 22, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment