Mwalimu wa shule ya
sekondari ya Nyakisasa iliyopo mkoani Kagera aliyetambulika kwa majina ya
Deogratias Simon anashikiliwa na jeshi la polisi Kagera kwa tuhuma za kumkashfu
Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.
Mwalimu huyo anadaiwa kutenda kosa
hilo mwaka 2016 kupitia mitandao ya kijamii ambapo inadaiwa alikuwa akisambaza
ujumbe ambao polisi wanaona ulikuwa na lengo la kumchafua Rais Magufuli.
Jeshi la polisi Kagera litamfikisha
mahakamani mtuhumiwa huyo baada ya uchunguzi kukamilika ili kumshtaki kwa kosa
hilo analodaiwa kulifanya mwaka 2016.
Mwalimu ashikiliwa na polisi kwa kumkashifu Raisi Magufuli
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 22, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment