Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye
amezungumzia tukio la kutishiwa bastola wakati akitaka kuzungumza na waandishi
wa habari nje ya Hoteli ya Protea lililotokea baada ya kuachwa katika
mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri
Katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa
Twitter, Nape amekumbushia tukio hilo la Machi 23, 2017 na kuandika, “mwaka
mmoja uliopita tarehe kama ya leo Mwenyezi Mungu aliniokoa na mdomo wa bunduki
wa wanyama wasiopenda haki! Mungu mkubwa, mbegu ya haki haifi.”
Katika ujumbe huo Nape aliweka picha yake ya video akizungumza na waandishi wa habari nje ya hoteli hiyo kueleza masuala mbalimbali, huku akiwataka vijana kudai haki zao bila woga.
Mtu aliyemtishia bastola Nape alikuwa pamoja na wenzake wawili ambao kwa pamoja walikuwa wakimlazimisha arudi kwenye gari lake na kuondoka, lakini mbunge huyo aligoma na ndipo (mtu huyo) aliporudi nyuma na kuchomoa bastola kutoka kiunoni kisha kumtishia kabla ya kutulizwa na mwezake.
Baada ya tukio hilo watu hao walitoweka eneo hilo muda mfupi baadaye.
Kufuatia tukio hilo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba alisema mtu aliyemtishia bastola Waziri huyo wa zamani wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo hakuwa askari wa Jeshi la Polisi.
NAPE AKUMBUKA ALIVYOKOSWA KUPIGWA RISASI HADHARANI
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 24, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment