HALMASHAURI YABAINI VIKUNDI HEWA 24

Halmashauri ya wilaya ya Hai Mkoa wa Kilimanjaro, imebaini vikundi hewa 24 kati ya 35 vilivyoomba mkopo wa asilimia tano unaotolewa kwa vikundi vya akinamama na vijana kwa lengo la kuwakwamua kiuchumi.

Mikopo ya aina hiyo hutolewa na halmashauri zote nchini.
Akizungumza jana Ijumaa Machi 23, 2018 mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Yohana Santoo ametoa kauli hiyo katika hafla fupi ya kukabidhi hundi ya Sh30milioni kwa vikundi 11 vya wajasiriamali wanaojishughulisha na kilimo, ufugaji na biashara

Amesema kati ya vikundi 35, 24 vimeondolewa kutokana na kubainika kwamba vilifanya udanganyifu

Amesema  baada ya kamati ya mikopo kubaini kasoro katika vikundi hivyo, wameviondoa kwa kukosa sifa

“Tulipokea vikundi 35 kati ya hivyo vikundi 11 ndivyo vilivyoonekana kuwa na sifa ya kupewa mikopo hii, vikundi 24 vimeonekana kutokuwa na sifa,”alisema

Mkurugenzi huyo amemwagiza ofisa maendeleo ya jamii pamoja na wataalam wake, kuhakikisha wanakwenda kutoa elimu kwa jamii kuhusiana na utoaji wa mikopo na vigezo vinavyotakiwa

Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo, Helga Mchomvu amesema kuwa fedha hizo zinatokana na asilimia 10 ya makusanyo ya mapato ya ndani
HALMASHAURI YABAINI VIKUNDI HEWA 24 HALMASHAURI YABAINI VIKUNDI HEWA 24 Reviewed by KUSAGANEWS on March 24, 2018 Rating: 5

No comments: