Halmashauri ya wilaya ya Hai Mkoa wa
Kilimanjaro, imebaini vikundi hewa 24 kati ya 35 vilivyoomba mkopo wa asilimia
tano unaotolewa kwa vikundi vya akinamama na vijana kwa lengo la kuwakwamua
kiuchumi.
Mikopo ya aina hiyo hutolewa na halmashauri zote nchini.
Akizungumza jana Ijumaa Machi 23, 2018 mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Yohana Santoo ametoa kauli hiyo katika hafla fupi ya kukabidhi hundi ya Sh30milioni kwa vikundi 11 vya wajasiriamali wanaojishughulisha na kilimo, ufugaji na biashara
Amesema kati ya vikundi 35, 24 vimeondolewa
kutokana na kubainika kwamba vilifanya udanganyifu
Amesema baada ya kamati ya mikopo
kubaini kasoro katika vikundi hivyo, wameviondoa kwa kukosa sifa
“Tulipokea vikundi 35 kati ya hivyo vikundi
11 ndivyo vilivyoonekana kuwa na sifa ya kupewa mikopo hii, vikundi 24
vimeonekana kutokuwa na sifa,”alisema
Mkurugenzi huyo amemwagiza ofisa maendeleo
ya jamii pamoja na wataalam wake, kuhakikisha wanakwenda kutoa elimu kwa jamii
kuhusiana na utoaji wa mikopo na vigezo vinavyotakiwa
Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo, Helga Mchomvu amesema kuwa fedha hizo zinatokana na asilimia 10 ya makusanyo ya mapato ya ndani
HALMASHAURI YABAINI VIKUNDI HEWA 24
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 24, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment