MAWAZIRI WA AFYA NCHI TISA KUTOA MAPENDEKEZO YA KUPAMBANA NA EBOLA

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, amewataka Mawaziri wa Afya kutoka nchi tisa za Afrika kutoa mapendekezo ya namna ya kutokomeza magonjwa yasiyoambukiza kwa wakuu wa nchi hizo ili yafanyiwe kazi.
Aliyasema hayo juzi wakati akifungua Mkutano wa 65 wa Mawaziri wa Afya kutoka nchi tisa wanachama wa Jumuiya ya Afya kwa nchi za Afrika Mashariki, Kati  na Kusini (ECSA-HC)
Alisema magonjwa yasiyoambukiza ni miongoni mwa magonjwa ambayo yameendelea  kuwatesa wananchi kwa kiasi kikubwa katika nchi nyingi za Bara la Afrika, hivyo vema mawaziri hao wakati mapendekezo ya namna ya kuyatokomeza.
Alisema magonjwa hayo yanaweza kudhibitiwa kwa kuhamasisha wananchi kuboresha lishe na kusisitiza ulaji wa vyakula bora, kufanya mazoezi na kubadili mitindo ya maisha.

“Magonjwa yasiyoambukiza yanaongoza kwa kusababisha vifo katika baadhi ya nchi wanachama wa ECSA. Magonjwa haya yanachangiwa kwa kiasi kikubwa na mabadiliko ya mfumo wetu wa lishe na maisha, hivyo ni muhimu suala hili likatafutiwa ufumbuzi.”

Waziri Mkuu alisema magonjwa yasiyoambukiza pamoja na magonjwa mengine ya milipuko kama ebola, homa ya bonde la ufa, dengue, homa ya manjano yamekuwa kikwazo cha maendeleo katika baadhi ya nchi.
MAWAZIRI WA AFYA NCHI TISA KUTOA MAPENDEKEZO YA KUPAMBANA NA EBOLA MAWAZIRI WA AFYA NCHI TISA KUTOA MAPENDEKEZO YA KUPAMBANA NA EBOLA Reviewed by KUSAGANEWS on March 21, 2018 Rating: 5

No comments: