Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA) kupitia Katibu Mkuu wake Dkt. Vicent Mashinji amesema
wanafanyiwa usumbufu na Jeshi la Polisi wa kuitwa kila wiki na mwishowe hakuna
jambo jipya wanaloambiwa wanapokuwa wameitikia wito wa kuripoti.
Dkt. Vicent Mashinji ametoa kauli
hiyo muda mchache alipotoka nje ya kituo cha Polisi 'Central' Jijini Dar es
Salaam leo (Machi 22, 2018) baada ya kuitikia wito wa Kipolisi kama
walivyotakiwa kufanya hivyo awali kwa lengo la kuhojiwa juu ya tuhuma za
kufanya mkusanyiko usiokuwa halali.
"Jambo moja nataka niwakumbushe
watanzania wenzangu kwamba Tanzania tunakitu kinachoitwa kiingereza 'Police
Force' hatuna 'Police services' yaani maana yake tuna Jeshi la Polisi la
kusukuma watu nasio la kutoa huduma mbalimbali kwa jamii", amesema Dkt. Mashinji.
Pamoja na hayo, Dkt. Mashinji
ameendelea kwa kusema "kila bada ya siku tatu nne tunakuja,
tunakaa hapa hakuna jambo lolote la maana linalofanyika kwa hiyo inaonekana tu
kwamba ni usumbufu tu. Muda mwingine mtu anapoamua kukusumbua tu unampa fursa
tu naye ajisikie tu raha afanye kile anachojisikia, kimsingi hakuna jambo
lolote tunalolivunja kisheria zaidi ya wao ya usumbufu mara kwa mara. Sisi
tutaendelea kuripoti kulingana na wao wanavyotaka".
Kwa upande mwingine, viongozi wa
CHADEMA wametakiwa kurudi tena kituo cha Polisi Jijini Dar es Salaam siku ya
Jumanne Machi 27 mwaka 2018.
MASHINJI ASEMA JESHI LA POLISI WANAWASUMBUA SANA
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 22, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment