Polisi mkoani Shinyanga wanamshikilia mzee
mwenye umri wa miaka 90, Kachuka Malongo kwa tuhuma za kubaka wanafunzi watano
wa Shule ya Msingi Tinde, Wilaya ya Shinyanga
Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari jana
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Simon Haule alisema kwamba wanafunzi
hao walibakwa kwa nyakati tofauti na mtuhumiwa akiwarubuni kwa kuwapa pipi na
pesa
“Tumebaini chanzo cha tukio hilo kuwa ni
tamaa na uchu wa mapenzi. Tayari tunamshikilia mtuhumiwa kwa mahojiano zaidi na
uchunguzi ukikamilika tutampeleka mahakamani,” alisema Kamanda Haule
Akizungumzia tukio hilo Kamanda Haule
alisema kwamba mkazi wa Tinde, Amada Mganyizi ndiye aliyebaini kubakwa kwa
wanafunzi hao Machi 21 saa 2:30 asubuhi. Hata hivyo, hakueleza kwa undani namna
gani mkazi huyo alibaini kubakwa kwa watoto hao.
Alisema kwamba wanafunzi hao ambao majina
yao yanahifadhiwa wana umri wa kati ya miaka minane na 12 na wanasoma katika
shule za msingi Tinde A na B.
“Natoa rai kwa wananchi na wazazi kuwa
makini na karibu na watoto wao ili kubaini mabadiliko yao. Lakini kitu kingine
kikubwa, nawataka wachukue hatua za haraka wanapobaini watoto wamefanyiwa
ukatili kama huu,” alisema
Kamanda huyo.Aliwaonya watu wazima wenye tabia hizo kuacha mara moja.Baadhi ya wananchi wa Tinde A waliohojiwa kuhusu tukio hilo walisema endapo itabainika kwamba ni kweli kwamba mzee huyo amefanya hayo, achilia mbali kuwa kitakuwa ni kitendo cha ukatili, pia kitakuwa ni cha aibu kufanywa na mzee wa umri huo
Hussein Seif alisema wamesikitishwa na
taarifa za mzee huyo kuhusishwa na kitendo cha kubaka wajukuu wake
Kikongwe wa miaka 90 adaiwa kubaka watoto watano
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 25, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment